Rais Joseph Kabila
Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo leo anatarajiwa kumteua Waziri Mkuu, licha ya upinzani ambao ulipaswa kutoa jina hilo, kugawanyika, juu ya nani atakayeteuliwa.


Mpaka sasa upinzani umegawanyika pande mbili, ukiwemo ule unaopinga kuteuliwa kwa Felix Tshekedi licha ya kuongoza kundi kubwa na upande mwingine ni wanaomuunga aliyekuwa mshauri mkuu wa marehemu Tsichekedi ambaye alifukuzwa kwenye chama hicho, baada ya kufanya mazungumzo na Rais Kabila.

Hata hivyo kwa mujibu wa rais kabila, kuteuliwa kwa waziri mkuu mpya ni kutatatua mvutano uliozuka, kuhusu utekelezaji wa makubaliano ya tarehe 31 Desemba mwaka jana, makubaliano ambayo yanataka waziri mkuu atoke upande wa Muungano wa upinzani. 

Lakini hadi sasa bado hawajaafikiana kuhusu namna ya kufanya uteuzi, kutokana na mgawanyiko ulitokea upande huo wa upinzani baada ya kifo cha marehemu mkogwe wa upinzani Etienne Tshisekedi, ambae alikuwa anaongoza muungano huo, licha mtoto wake kuteuliwa kuchukuwa nafasi yake hiyo.

Aliyekuwa waziri Mkuu wa DRC, Samy Badibanga.
Hatua hii inafuatia aliyekuwa waziri mkuu katika Jamhuri ya Kidemokrasia  ya Congo Samy Badibanga kujiuzulu kama sehemu ya makubaliano yaliyoongozwa na kanisa katoliki kumaliza mzozo wa kisiasa nchini humo.

Kwa upande wake Rais Joseph Kabila, aliwaambia wabunge wa nchi hiyo kuwa atamteua waziri mkuu kutoka upinzani ndani ya saa 48 zinazokuja.

Bwana Kabila alisema kuwa atafuata tararibu zilizoafikiwa kama sehemu ya makubaliano na upinzani ambayo yanataka uchaguzi kuandaliwa kabla ya mwisho wa mwaka huu.

Chanzo:  BBC Swahili News.
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top