Wachazeji wa mpira wa Kikapu nchini New Zealand

Mchezaji wa mpira wa kikapu nchini New Zealand Akil Mitchell amesema anapata nafuu baada ya jicho lake kutoka alipokuwa uwanjani akicheza.


Mitchell huchezea klabu ya New Zealand Breakers, na alikuwa mjini Auckland kucheza mechi ya NBL ya Australia Alhamisi usiku kisa hicho kilipotokea.

Mchezaji wa timu pinzani aliingiza kimakosa kidole ndani ya tundu la kishimo cha jicho na ghafla jicho lake likatoka nje.

Mchezaji huyo mzaliwa wa Marekani alianguka sakafuni akiwa ametumia mikono yake kufunika jicho lake la kushoto na akakimbizwa hospitalini.

"Kwa viganja vya mkono wangu, nilihisi mboni ya jicho ikiwa nje na kukaa upande mmoja wa uso," aliambia Radio Sport ya New Zealand.

"Bado jicho hilo lilikuwa linaona."

"Nakumbuka nikifikiria, bwana we ... hii ni hali mbaya, lakini nilihisi kwamba lilikuwa jambo la kushangaza na hapo ndipo niliingiwa na wasiwasi kiasi."

Chanzo:  BBC News


Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top