Jengo la Idara Kuu ya Usalama nchini Russia.
Russia imemfukuza nchini wakala wa kijasusi aliyekuwa akifanya kazi kwa ajili ya mashirika ya kijasusi ya Marekani na Latvia kwa wakati mmoja kwa zaidi ya miongo miwili.

Mtu huyo alikuwa akikusanya taarifa za kijeshi kwa ajili ya mashirika ya kijasusi ya Marekani na Latvia. 

Shirika la Ujasusi la Russia limemtaja Andrejs Dudarevs inspekta wa ngazi ya juu wa shirika la anga la Latvia kama wakala wa kijasusi aliyekuwa akitumikia nchi mbili na hivyo kumpiga marufuku kuingia Russia kwa miaka kumi. 

Kanali ya habari ya Russia ya NTV imetangaza kuwa Dudarevs aliyafanyia kazi mashirika ya kijasusi kwa muda wa miaka 22, ambapo kwa mara ya kwanza aliifanyia ujasusi Latvia na kisha Marekani, huku akizikusanyia nchi mbili hizo taarifa zinazoihusu Wizara ya Ulinzi ya Russia. 

Mwaka 2011 jasusi huyo alijaribu kuwasiliana na idara za usalama za Russia na miaka mitatu baadaye, alikutana na wawakilishi wa shirika la ujasusi la Russia akiomba kazi katika sekta ya masuala ya anga ya kijeshi, mkabala na kuvujisha taarifa kuhusu mawakala wenzake wa Magharibi na kwa ajili ya maslahi mengine ya kifedha.

Chanzo:  Sauti ya Radio Iran.
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top