Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju (katikati) akizungumza na viongozi wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited alipotembelea makao makuu ya kampuni hiyo Tabata Relini, Dar es Salaam. Picha kwa hisani ya Mwananchi. 

Maneno haya machache yamenakiliwa kutoka Gazeti la Mwananchi, ambayo yalitamkwa na mwanasheria mkuu wa serikali nchini, George Masaju alipozungumza na uongozi wa gazeti hilo hivi karibuni.


Ki ukweli Madhehebu yote ya dini nchini ukiachilia mbali Uislamu yana taasisi zake mbalimbali na zote zimesajiliwa na zinatambuliwa na serikali, leo mwanasheria kudai serikali inaitambua BAKWATA peke yake, ni wazi taasisi nyingine zilipatiwa usajili FEKIIII!! Soma mwenyewe alivyofafanua siku hiyo:-

"Kuhusu kugawanyika kwa Waislamu katika kulitambua Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Masaju alisema hakuna jinsi ya kulikwepa baraza hilo kwa kuwa ni chombo kinachotambuliwa na Serikali kisheria.

“Kwanza kwa mfumo wetu wa sheria, taasisi ile ya BAKWATA ndio inayotambulika kabisa kisheria, hivyo endapo wapo wanaoipenda au wasioitaka, hakuna jinsi ya kuikwepa” alisema.

Lakini akasema kuwa katika suala hilo, Waislamu wote waliungana na kuwa na msimamo mmoja.

“Na sisi tunacholenga kama serikali ni kuhakikisha kuwa watu wote katika jamii wanakuwa na amani,” alisema.

Alisema kuwa walikutana na viongozi hao wa Kiislamu Februari 3 na walikiri kuwapo na tofauti, lakini wakasema tofauti walizokuwa nazo wameziondoa na wameungana kutokana na umuhimu wa kuwapo kwa mahakama hiyo.

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top