BANA ALABED - AMWANDIKIA BARUA RAIS TRUMP.
Bana Alabed, msichana wa miaka saba kutoka Aleppo ambaye alipata umaarufu duniani kutokana na ujumbe ambao alikuwa akiandika kutoka Aleppo, amemwandikia Rais Donald Trump barua ya wazi.


"Lazima uchukue hatua kuhusu watoto wa Syria kwani ni sawa na watoto wako mwenyewe na wanahitaji amani kama wewe mwenyewe," ameandika.

"Nikiwa Aleppo sikuweza kucheza. Aleppo ulikuwa mji wa mauti."

Bana alifanikiwa kuondoka Aleppo pamoja na familia yake Desemba wakati wa mpango mkubwa wa kuwaondoa raia maeneo yaliyodhibitiwa na waasi.

Kwa sasa anaishi Uturuki.

Ukurasa wake wa Twitter ulipata umaarufu sana kutokana na ujumbe alioandika akiwa maeneo ya mashariki mwa Aleppo wakati maeneo hayo yalikuwa yamezingirwa na wanajeshi wa serikali.

Mamake, Fatemah - ambaye amekuwa akimsaidia kuandika ujumbe kwenye ukurasa huo wake - ametuma nakala ya barua hiyo kwa BBC.

Anasema Bana aliandika barua hiyo siku kadha kabla ya Trump kuapishwa kuwa rais, kwa sabbau alikuwa "anamuona Trump mara nyingi kwenye runinga.

Chanzo:  BBC News
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top