Katibu Tawala mkoani Shinyanga (RAS) Abdul Dachi  (kushoto) akiwasili katika ofisi za TUGHE mkoani Shinyanga,  kulia ni katibu wa TUGHE mkoani Shinyanga, Tabu Mambo na Mwenyekiti wa TUGHE mkoa, John Mfutakamba wakimpokea.
 
Hapa anasalimiana na baadhi ya viongozi wa matawi ya TUGHE mkoani Shinyanga.




CHAMA Cha wafanyakazi wa Serikali kuu na Afya Tanzania (TUGHE) mkoani Shinyanga kimelalamikia kitendo cha baadhi ya waajiri katika idara za serikali kuzuia kufanyika kwa vikao vya mabaraza ya wafanyakazi kwa mujibu wa sheria.


Hali hiyo imetajwa kushusha ari ya wafanyakazi kufanya kazi katika sehemu za kazi kutokana na kukosa eneo la kuzungumzia changamoto mbalimbali zinazowakabili na kwamba moja ya kazi ya mabaraza ni kuishauri menejimenti juu ya mambo muhimu yanayohusu maslahi ya wafanyakazi.

Akisoma risala ya viongozi wa TUGHE juzi kwa katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga (RAS), Abdul Dachi ambaye ndiye mwajiri mkuu wa watumishi wa serikali, katibu wa TUGHE mkoani humo, Tabu Mambo alisema baadhi ya ofisi za serikali haziruhusu kufanyika kwa vikao vya mabaraza ya wafanyakazi.

Akielekea katika ukumbi wa mikutano akiongozwa na mwenyekiti wa TUGHE mkoa.
Alisema kutofanyika kwa vikao hivyo kunawanyima haki wafanyakazi kufahamu bajeti ya taasisi husika na hivyo kusababisha kuwepo kwa malalamiko wakati wa utekelezaji wake pamoja na kwamba mabaraza hayo yameundwa kwa mujibu wa sheria.

Mambo alifafanua baadhi ya changamoto zinazowakabili watumishi wa umma ni kima kidogo cha mishahara ambacho hakikidhi mahitaji ya mwezi mzima ya mfanyakazi ikiwemo makato makubwa ya kodi inayokatwa kila mwezi ambapo walishauri makato hayo yapunguzwe.


Hapa ni wimbo wa Mshikamano (Solidarity)
Hapa mgeni rasmi anaweka saini yake katika kitabu cha wageni.
Kwa upande wake mwenyekiti wa TUGHE mkoani Shinyanga, John Mfutakamba alimweleza katibu tawala huyo kwamba pamoja na changamoto zinazowakabili watumishi wa umma watahakikisha wanatimiza wajibu wao kikamilifu ili uchumi wa nchi usiporomoke.

Mwenyekiti wa TUGHE Mkoa akitoa neno kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzungumza na viongozi wa matawi ya TUGHE Shinyanga

Viongozi wa matawi ya TUGHE wakimsikiliza mgeni rasmi.
“Mheshimiwa mgeni rasmi, pamoja na changamoto ulizoelezwa hapa, lakini napenda kukuhakikishia kwamba tutaendelea kuchapa kazi kwa bidii na uaminifu mkubwa chini ya rais ajaye wa awamu ya tano atakayechaguliwa, maana sisi kama watumishi wa umma tunaelewa dhamana tuliyonayo,”

“Dhamana ya uchumi wa nchi imo mikononi mwetu, ni wazi tunapaswa kutimiza wajibu wetu kikamilifu, tutakuwa makini katika maeneo yetu ya kazi na tunaamini hatutazembea, lakini pia tutatumia vikao vyetu vya TUGHE katika kujadiliana juu ya uboreshaji wa hali bora ya kazi katika maeneo yetu,” alieleza Mfutakamba.


 
Katibu Tawala mkoani Shinyanga akizungumza na viongozi wa matawi ya TUGHE Shinyanga.
Kwa upande wake katibu tawala aliwahakikishia viongozi hao kwamba ofisi yake itajitahidi kushughulikia changamoto zote zilizopo ili kuwawezesha wafanyakazi kufanya kazi zao kwa hali ya amani na utulivu na kwamba maeneo yote yenye mabaraza ya wafanyakazi vikao vyote vya kisheria vitakuwa vikifanyika.

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top