Mgombea mwenza wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (CCM), Bi. Samia Suluhu Hassan.
 
 
 
HII NYOMI NI YA ENEO MOJA TU, HAPA NI KATA YA BUZA, TEMEKE.
MGOMBEA Mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan amewaomba wakazi wa majimbo manne ya uchaguzi jijini Dar es Salaam waendelee kukichagua Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa vile ndiyo chama pekee chenye uwezo wa kuwaletea mabadiliko ya kweli. 
Bi. Hassan aliyasema hayo  kwa nyakati tofauti katika mikutano ya hadhara ya kampeni za kumnadi mgombea urais wa CCM, Dkt. John Magufuli uliyofanyika katika majimbo ya Kibamba, Ubungo, Kinondoni na Kawe.
 
Akiwa katika jimbo jipya la Kibamba, aliwataka wakazi wa jimbo hilo kuhakikisha hawarejei kosa walilolifanya mwaka 2010 kwa kumchagua mbunge anayetokana na upinzani, John Mnyika (CHADEMA) kwa vile tayari wamejionea uwezo wake mdogo wa kuwatumikia.
 
Alieleza kushangazwa kwake na madai ya wagombea wa upinzani ambao kila siku wanawashinikiza watanzania kukiondoa madarakani Chama cha Mapinduzi ili wao waweze kuleta mabadiliko na kwamba uwezo huo hawana na hawajawahi kuongoza nchi hata siku moja kwamba mabadiliko wanayoyataka wao ni yale ya kuleta machafuko.
 
“Ndugu zangu wakazi wa jimbo jipya la Kibamba, CCM tunapita kwenu kukuombeni kura zenu hapo Oktoba 25, mwaka huu, tunafanya hivi kwa vile tunawathamini, kikubwa tunachowaomba tupeni kura za kishindo kwa kumchangua mgombea urais wetu, Dkt. John Magufuli,”
 
“Lakini niwatahadharishe na kauli za wenzetu hawa wanaojiita UKAWA, wanapita wakiwaomba mfanye mabadiliko, waulizeni wanataka mabadiliko gani, maana tayari CCM imeshafanya mabadiliko makubwa katika nchi yetu, mfano mzuri ni mabadiliko ya kutoka mfumo wa chama kimoja na kuwa wa vyama vingi,”
 
“Niwahakikishie mabadiliko ya kweli yataendelea kuletwa na serikali ya CCM ndiyo yenye uzoefu, ninyi wenyewe ni mashahidi, linganisheni hali ya barabara zetu miaka 10 nyuma na zilivyo hivi leo, nyingi zimejengwa kwa kiwango cha lami, na hata kwenye bajeti zetu, tumeanza kubadilika, tumepunguza kutegemea wahisani,” alieleza Bi. Hassan.
 
Kwa upande wa jimbo la Ubungo, Bi. Hassan aliwahakikishia wakazi wa jimbo hilo iwapo serikali ya awamu ya tano chini ya Dkt. Magufuli itafanikiwa kuingia madarakani moja ya vipaumbele vyake vya kwanza ni kujenga hospitali kubwa ya kisasa katika jimbo hilo.
 
Kuhusu tatizo la ajira kwa vijana, alisema serikali ya awamu ya tano itafanya kila linalowezekana ili kumaliza tatizo la ajira kwa vijana kwa kufufua viwanda vilivyofungwa na kujenga vipya ili kuwezesha vijana kupata ajira na pia kuwezesha akinamama na vijana kupata mikopo yenye masharti nafuu ili kuinua mitaji yao.
 
“CCM hivi sasa imejipanga vizuri katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa ajira, moja ya mipango yetu ni kujenga viwanda vingi na kuvifufua vilivyofungwa ili vijana wetu wapate ajira, lakini pia tutafungua mfuko maalumu wenye kiasi cha shilingi milioni 10 utakaokuwa dhamana ya mikopo kwa vijana na akinamama,” alieleza Bi. Hassan.
 
Aidha kuhusu kero ya uhaba wa maji katika jiji la Dar es Salaam, alisema Chama cha Mapinduzi kinalielewa vyema tatizo hilo na hivi sasa kinafanya kila linalowezekana  kuhakikisha kero hiyo inatatuliwa na jiji la Dar es Salaam kwa kuongeza upatikanaji wake kutoka asilimia 75 ya sasa na kufikia asilimia 95.
 
Kwa upande wake Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki aliwaeleza wakazi wa kijiji cha Mloganzila waliokubali kuyahama maeneo yao kupisha ujenzi wa hospitali kubwa ya kisasa ili kuipunguzia mzigo hospitali ya Muhimbili kwamba serikali ya CCM imekubali pamoja na kulipwa fidia zao lakini pia watalipwa kifuta jasho kingine.
 
Mgombea mwenza huyo leo hii anaendelea na ziara ya mikutano ya kampeni katika wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam ambako ataendelea kumnadi mgombea urais wa CCM, Dkt. Magufuli, wabunge na madiwani wote wa CCM ambapo kwa jana aliweza kuhutubia mikutano minne ya kampeni.

Naye mgombea ubunge katika jimbo la Ubungo, Didas Masaburi alisema iwapo atachaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo, atahakikisha anavisaidia vikundi vya akina na mikopo (SACCOS) viweze kuimarka zaidi ambapo atatoa kiasi cha shilingi milioni 10 kwa kila SACCOS iliyopo katika jimbo lake.
 
M
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top