Bango la Taasisi ya Aziz Mahmud likiwa limefungwa eneo la machinjioni palikofanyika shughuli za uchinjaji.

Mmoja wa wasimamizi wa shughuli za uchinjaji na  mjumbe wa Taasisi ya Aziz, Bw. Hamad Al- Maamar akionesha ng'ombe 50 waliotolewa na taasisi yake kwa ajili ya kutolewa sadaka ya IDD EL HAJJ.
 
Mmoja wa viongozi wa Taasisi ya Aziz Mahmud Hudayi Wakf, Bw. Nuredolin Rustemor (mwenye miwani) akiomba dua maalum kabla ya shughuli ya uchinjaji kuanza rasmi, kulia kwake ni mchinjaji kutoka BAKWATA Shinyanga, Bw. Mbarak akisubiri kuchinja.
     
  










Kazi ya uchinjaji na uchunaji ikiendelea eneo la machinjio Shinyanga mjini.

 
Hapa baadhi ya viongozi wakiandika utaratibu wa usambazaji wa sadaka hiyo kwenda kwenye vituo mbalimbali mjini Shinyanga

Moja ya gari kutoka kituo cha Mhumbu Islamic Shinyanga likiwa tayari kubeba msaada wa nyama kwenda kituoni.

TAASISI ya Aziz Mahmud Hudayi Wakf  (Rehema Friendship and Solidarity Trust (REFSO) yenye makazi yake jijini Dar es Salaam imetoa sadaka ya ng’ombe 50 wenye thamani ya shilingi milioni 30 kwa makundi mbalimbali ya watu wasio na uwezo wakiwemo walemavu wa ngozi waliopo katika kituo cha Shule ya msingi Buhangija Jumuishi Shinyanga.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaji wa taasisi hiyo, Hussein Mohamed, sadaka hiyo imetolewa ikiwa ni katika kuwakumbuka watu wasio na uwezo ili wa mjini Shinyanga nao waweze kusherehekea vizuri siku kuu ya Idd el Hajj ambayo huambatana na sadaka ya kuchinja.

“Huu ni mwaka wa pili tumekuwa tukitoa sadaka hii katika baadhi ya mikoa hapa nchini, lengo letu ni kuwasaidia watu wasio na uwezo waweze kupata kitoweo katika siku kuu hii ya Idd el Hajj ambayo huadhimishwa na waumini wa kiislamu ulimwenguni kote ikienda sambamba na sadaka ya kuchinja,”

“Kwa hapa Shinyanga mwaka huu sadaka hii itatolewa kwa makundi mbalimbali ikiwemo vituo vinavyotunza watoto yatima na kile cha Buhangija kwa watoto wenye ulemavu wa ngozi (albinism), pia msaada kama huu umetolewa katika mikoa  mingine nchini,” alieleza Mohamed.

Mbali ya sadaka hiyo kupelekwa kwa makundi ya watu wasio na uwezo pia itatolewa kwa waumini mbalimbali wa kiislamu waliopo kwenye misikiti ya mjini Shinyanga na kwamba zaidi wa waumini 1,000 wanatarajiwa kupata sadaka hiyo ya EID EL HAJJ.

Septembar 24, 2015.
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top