Muungano wa mashirika ya haki za binaadamu
nchini Kodivaa yameingiwa na wasiwasi juu ya nchi hiyo kutuma askari wake
kwenda kuungana na vikosi vya nchi nyengine za magharibi mwa Afrika kupambana
na kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram nchini Nigeria.
Muungano huo ulitangaza kuwa badala ya serikali ya Yamoussoukro kutuma askari
wake kupambana na kundi hilo, inatakiwa kujikita katika kudhamini usalama na amani
kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao.
Aidha muungano huo umesisitiza kuwa, wananchi
wa Ivory Coast wana wasiwasi kwamba, hali inaweza kuwa tete kiusalama na
kisiasa ikiwa askari wa nchi hiyo watatumwa kupambana na Boko Haram.
Umeongeza kuwa, wanakubaliana na suala la
kupambana na wanamgambo wa kundi hilo, lakini hali inayotawala kwa sasa Kodivaa
hairuhusu kujiingiza katika vita vingine.
Mwezi uliopita Rais Alassane Ouattara
alitangaza azma ya nchi yake kutuma askari wake mwezi huu wa Aprili kwa ajili
ya kujiunga na muungano wa kieneo unaopambana na Boko Haram.
Source: Radio
Tehran
Soma Pia Habari Hizi Hapa
- HABARI ZA HIVI PUNDE: PAPA FRANCIS ATEMA "CHECHE" VATICAN, ATETEA AFYA ZA WAUMINI10 Nov 20170
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...Read more ?
- KIVULINI WAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA KIKE KWA KUTOA MAFUNZO KWA WANAMABADILIKO - SHINYANGA.11 Oct 20170
Normal 0 false false false MicrosoftInternetExplorer4...Read more ?
- WANA CHADEMA KANDA YA SERENGETI WATOA TAMKO LA KUMLAANI MTU ASIYEJULIKANA10 Sep 20170
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...Read more ?
- MAAJABU YA DUNIA, ETI MBU NAO HUVUTIWA NA VITU VITAMU!!!24 Aug 20170
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...Read more ?
- BREAKING NEWS: MOTO WATEKETEZA MABANDA YA MBAO SHINYANGA29 Apr 20170
Moja ya banda la kuuzia mbao katika eneo la Soko la Kambarage manispaa ya Shinyanga likiwa lote ...Read more ?
- HABARI NYEPESI NYEPESI: BAADA YA HALI KUWA NGUMU, WAZAZI SASA KULIPA KARO ZA SHULE KWA MBUZI NA KONDOO!!23 Apr 20170
Normal 0 21 false false false SW X-NONE X-NONE ...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.