Waziri wa Ujenzi, John Magufuli.
Waziri wa Ujenzi, John Magufuli ameupongeza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad) kwa kuwachukulia hatua watendaji wa Kampuni ya Dott Services kwa kosa la kuchelewesha ujenzi wa barabara ya Mkumbara hadi Same yenye urefu wa kilomita 96.


Kampuni hiyo yenye makao yake makuu nchini Uganda, imeshindwa kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo unaogharimu Sh103.8 bilioni huku kampuni ya Strabag iliyochukua ukandarasi wa kujenga barabara kama hiyo ya Korogwe hadi Mkumbara, ikimaliza kazi yake Desemba 3, mwaka jana kama ilivyosaini mkataba.

Dk Magufuli alitoa pongezi hizo wakati akikagua barabara hizo baada ya Mtendaji Mkuu wa Tanroad, Patrick Mfugale kuelezea kwamba alilazimika kuwafukuza baadhi ya mameneja wa Kampuni ya Dott Services wanaodaiwa kusababisha isikamilike kwa wakati.

Alisema kampuni hiyo ilishalipwa Sh44.5 bilioni za awali kama mkataba unavyoelekeza na kutakiwa kukamilisha ujenzi kwa asilimia 67 kabla ya kulipwa fedha zingine.

Hata hivyo, Mfugale alisema Kampuni ya Strabag iliyojenga barabara ya Korogwe hadi Mkumbara yenye urefu wa kilomita 76 kwa Sh87.8 bilioni, imeishakabidhi na kwasasa iko chini ya uangalizi hadi Desemba, mwaka huu. “Barabara hii iko chini ya uangalizi hadi Desemba, mwaka huu, tunalenga kubaini kama kuna upungufu uweze kurekebishwa,” alisema Mfugale.

Source: Mwananchi News

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top