Viongozi wakuu wa CCM Taifa.
 
TAARIFA RASMI YA KIKAO
Kamati Kuu ya CCM (CC) inakutana Jumamosi Februari 28, 2015 huku mambo muhimu sita yakitarajiwa kujadiliwa, likiwamo suala la makada wa chama hicho waliopewa adhabu ya onyo kali kwa kuanza kampeni za urais mapema na ukiukaji wa maadili.


Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, licha ya kutoeleza ajenda za kikao hicho, ilisema kitafanyika jijini Dar es Salaam na kuongozwa na mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete kuanzia saa 4 asubuhi.

Kikao hicho kinafanyika wakati upepo wa kisiasa ndani ya chama hicho ukiwa haujatulia huku kukiwapo masuala mazito ya kitaifa yanayotikisa medani za kisiasa, likiwamo suala la uandikishaji wapiga kura, maandalizi ya kura ya maoni za kupitisha Katiba Inayopendekezwa na maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, ambayo yameelezwa na wachambuzi wa siasa kuwa hayawezi kukwepeka katika kikao hicho.

Adhabu kwa wagombea:

Itakumbukwa kuwa kikao hicho kitafanyika ikiwa ni siku 10 baada ya kukamilika tarehe ya mwisho ya adhabu kwa makada sita wa CCM, waliokuwa wakitumikia adhabu ya miezi 12 kwa ukiukwaji wa maadili kwenye mchakato wa kutaka kuteuliwa na CCM kugombea urais.

Kikao kilichopita cha CC kilichoketi Januari 13, mwaka huu kilibainisha kuwa baada ya muda wa adhabu zao kuisha, Kamati Kuu ingefanya tathimini kuona iwapo wagombea hao walizingatia masharti ya adhabu zao na endapo kungekuwa na ambao hawakuzingatia masharti  adhabu zao zingeongezwa.

Wiki iliyopita, Nnauye alithibitisha kuwa muda wa adhabu hiyo ulikuwa ukingoni na kuwa viongozi hao wangefanyiwa tathmini na kamati ndogo ya maadili ili kubaini iwapo adhabu hiyo ilitekelezwa ipasavyo.

Makada waliokuwa wakitumikia adhabu hiyo ni Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Waziri mkuu mstaafu, Frederick Sumaye.

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top