ALIUA MKE WA MTU NA YEYE AKAUAWA NA MWENYE MKE!!!
Miezi minne iliyopita, Demeteriya Nabire aliliwa na mamba alipokwenda mtoni karibu na makazi yake kuchota maji. Mnyama huyu alirudi tena baaae katika eneo lilelile na kumkuta mume wa Nabire anasubiri, tayari kwa kulipa kisasi.


Demeteriya Nabire alikuwa kwenye kingo za mto akiwa na wanawake wengine kutoka kwenye Kijiji anachoishi, walikuwa wakichota maji kutoka katika Mto Kyoga nchini Uganda, Mamba alifika na kumnyaka alimburuza kisha mwanamama huyu hakuonekana tena.

Mumewe, Mubarak Batambuze, aliingiwa na hofu sana, Nabire alikuwa mjamzito.hivyo Mubarak hakupoteza mkewe tu bali kiumbe kilichokuwa tumboni.alijihisi kukosa nguvu, lakini Mwezi uliopita akasikia kuwa Mamba amerejea.

''Mtu mmoja akaniita 'mubarak nina habari kwa ajili yako, Mamba aliyemchukua mkeo amerudi, tena'

Mvuvi huyo mwenye umri wa miaka 50 akaelekea mtoni na marafiki zake.'' alikuwa mkubwa, na tulijaribu kupambana nae kwa mawe na fimbo lakini hatukufanikiwa,'' alisema.

Hivyo Batambuze alienda nyumbani kwa muhunzi.

''Nikamweleza kuwa napambana na Mamba ambaye amenichukulia mke wangu na mtoto aliyekuwa tumboni.ninataka sana kulipa kisasi, kisha nikamwambia anitengenezee silaha ambayo ingeweza kumuua mamba huyo.

Mtu huyo alitaka nilipe kiasi cha pauni 3.20 ili atengeneze Mkuki.

Akiwa na mkuki wake mkononi alielekea kwenye mapambano.

Lakini alipofika kwenye maji, Mamba alikuwepo eneo hilo, lakini Marafiki wa Batambuze waliingiwa hofu na kumsihi asimshambulie kwa kuwa alionekana mkubwa sana na angeweza kumla, wakamwambia kuwa Mkuki huo hautafaa.

Batambuze akasisitiza waendelee kubaki, ''nilishindwa kumuua mwanzo, alisema,'' sioni tatizo nikifa wakati namuua Mamba natatumia mkuki huu, na nitahakikisha amekufa''.

Ofisa wa wanyama pori Oswald Tumanya,  amesema kuwa Mamba alikuwa na urefu wa zaidi ya mita nne na uzito wa kilo 600.
 
''nilikuwa na wasiwasi sana lakini kilichonisaidia ni Mkuki, '' alisema Batambuze.

Alifunga kamba kwenye kwenye mkuki kwenye sehemu iliyotengenezwa mithili ya kisu kikali, ''niliweka silaha yangu eneo Mamba alipo huku marafiki zangu wakinisaidia kurusha mawe na kumchapa mamba mgongoni kwake wakitumia fimbo, Alijaribu kunyanyua mdomo wake juu ili anishambulie.''

Alishikwa na hasira sana, kisha kulikuwa na hofu sana katika eneo hilo, lakini nilikuwa na nia, na sikuhofu kufa, nilitaka kumuua hivyo nilirusha silaha yangu alipo mamba kisha nikavuta kamba. Mamba alianza kuwa matatani.''

Ilichukua saa moja na nusu mwa Batambuze na marafiki zake wakipambana na Mamba, hatimaye walifanikiwa kumuua.

Wakiwa wamechoka walirejea kijijini kwao ''kulikuwa na mshtuko mkubwa, kilichomshangaza kila mtu ni ukubwa wa Mamba, hakuwa mamba wa kawaida, alikuwa mkubwa sana. Na Watu wakatuita mimi na marafiki zangu mashujaa,'' alisema.

Chanzo:  BBC News!

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top