Mwenyekiti wa chama cha APPT-Maendeleo, Mhe Peter Mziray
Chama cha APPT Maendeleo, kimepinga hatua inayochukuliwa na baadhi ya vyama vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuwashawishi wananchi wasishiriki kupiga kura ya maoni kwa ajili ya kuamua Katiba inayopendekezwa.

 
Katibu Mwenezi wa APPT Maendeleo Taifa, Godfrey Davis, akizungumza na waandishi wa habari  amesema kuwashawishi wananchi wasishiriki kupiga kura, ni kosa na ni kuwanyima haki ya demokrasia ya kuamua Katiba yao.
 
Davis alisema vyama vya siasa vitambue kuwa mchakato wa Katiba umegharimu mamilioni ya fedha, hivyo ni jambo la kushangaza wakati imefikia hatua ya mwisho kisha wanashawishi wasishiriki wakati wanaopinga wanayo nafasi ya kupiga kura ya hapana.
 
Hata hivyo, alisema APPT Maendeleo inaungana na vyama vingine vya siasa kuitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kusogeza mbele zoezi la uandikishaji wapiga kura pamoja na kura ya maoni.
 
Alisema kimsingi muda uliobaki Nec haiwezi kukamilisha mchakato wa kuandikisha wapiga kura wote wenye sifa na kuingia katika upigaji kura ya maoni na kuleta ufanisi.
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top