Nyie hamfai mbele ya Jamii, lazima mtiwe hatiani!! bora ya huyu Hakimu!!!
Akikatisha tu!!! namvagaa!!! najipakulia kiulainiiiii!!!
 
Mhh!!! mbona haletwi mbakaji nitengeneze mihelaa hapa???
BAADHI ya wakazi wa mji wa Shinyanga wamevilalamikia vyombo vya sheria mkoani humo kutokana na jinsi vinavyopindisha kwa makusudi ushahidi wa kesi zinazohusiana na matukio ya ubakaji ikiwemo kulawiti hali inayochangia kuendelea kwa vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.
 
Hatua ya kulalamika kwa wakazi hao inatokana na Mahakama ya wilaya ya Shinyanga kumuachia huru bila masharti mshitakiwa wa kesi ya ubakaji Eugen Mwaluko (18) aliyekuwa ameshitakiwa kwa kosa la kumbaka mtoto mdogo mwenye umri wa miaka tisa anayesoma darasa la tatu ambaye pia anasumbuliwa na tatizo la ugonjwa wa kupanuka moyo.
 
Wakizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo wakazi hao wameelezea kutoridhishwa na hukumu hiyo na kwamba imeonesha wazi jinsi fedha ilivyotumika ambapo walidai kitendo cha ushahidi kutojitosheleza wakati mtoto anaonekana wazi kuharibiwa sehemu zake za siri na kutambuliwa kwa mshitakiwa ilitosha kuwa ushahidi.
 
Wakazi hao walisema ongezeko la vitendo vya kubakwa na kulawitiwa kwa watoto wadogo katika siku za hivi karibuni mkoani humo inaonesha wazi kunatokana na vyombo vya sheria kutokutoa adhabu kwa washitakiwa wanaokamatwa huku baadhi ya kesi nyingi zinazofikishwa mahakamani zikichukua muda mrefu bila sababu za msingi.
 
Mmoja wa wakazi hao aliyejitambulisha kwa jina la Njile Maganga mkazi wa Mwasele manispaa ya Shinyanga alisema tabia ya vyombo vya sheria kuharibu kwa makusudi kesi zinazohusiana na masuala ya kubakwa kwa watoto ndiyo chanzo cha mkoa wa Shinyanga kuongoza kwa matukio ya ukatili dhidi ya watoto kwa asilimia 59.
 
Maganga alisema mbali ya mkoa huo kuongoza kwa matukio ya ukatili wa kijinsia pia kwa mujibu wa utafiti ulioendeshwa na Shirika la Kimataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) watoto 16 hubakwa kila siku mkoani Shinyanga hali inayoonesha wazi ukubwa wa tatizo hilo la ukatili na unyanyasaji wa jinsia mkoani humo.
 
“Kwa kweli binafsi nimechanganyikiwa, maana inavyoelekea mkoa wetu sasa vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vinaonekana kuwa vya kawaida, kitu ambacho ni cha hatari kwa mstakabali wa wahanga wa matukio hayo, tulitegemea vyombo vya sheria vikomeshe hali hii, lakini na vyenyewe inaonekana kusaidia watuhumiwa,” alieleza Maganga.
 
Akizungumzia kufutwa kwa kesi hiyo, baba mzazi wa mtoto Novatus Ernest (42) mkazi wa Lubaga Farm Manispaa ya Shinyanga alisema ameshangazwa na jinsi hukumu hiyo ilivyotolewa na kwamba imeonesha wazi mahakama imeshindwa kumtendea haki mtoto wake.
 
“Kwa ujumla hivi sasa nimechanganyikiwa, maana pamoja na mwanangu kuharibiwa sehemu zake za siri lakini bado mahakama imemuachia huru mshitakiwa kwa madai ya kutopatikana kwa ushahidi wa kutosheleza pamoja na mtoto mwenyewe kumtambua mshitakiwa mahakamani,”
 
“Hivi sasa ninajipanga kukata rufaa, na ninaomba iwapo hapa nchini kuna wanaharakati wa kupinga ukatili dhidi ya watoto wanisaidie, maana haki ya mtoto wangu inachezewa wakati tayari ameishaathiriwa kisaikolojia na kuharibiwa sehemu zake za siri, ukweli haki haikutendeka, nimeamini nilichoelezwa na baba wa mshitakiwa kuwa nitaondoka patupu,” alieleza Novatus.
 
Hata hivyo kwa upande wake Hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Shinyanga aliyesoma hukumu hiyo, Neema Gasabile alikanusha madai ya kupindisha haki katika kesi hiyo na kwamba kuachiwa huru kwa mshitakiwa huyo kunatokana na upande wa mashitaka kushindwa kutoa ushahidi mahakamani hapo usioacha shaka.
 
“Ni kweli leo hii (jana) nimemuachia huru mshitakiwa aliyekuwa akishitakiwa katika kesi ya jinai namba 1 ya mwaka 2015, Eugene Mwaluko, hii ni baada ya kukosekana ushahidi unaomtia hatiani, hapakuwa na kesi ya kulawiti bali ilikuwa ni kesi ya kawaida ya ubakaji,”
 
“Katika kesi hii ushahidi wa mhanga (mbakwaji) ambao haukuwa wa kiapo kwa vile ni mtoto ulikosa ushahidi wa kuungwa mkono na hivyo kuacha shaka kwa upande wa mahakama, lakini pia maelezo yaliyoandikwa katika fomu namba tatu ya matibabu yalipingana na  aliyotoa daktari mahakamani hapa,” alieleza Gasabile.
 
Alisema baada kupingana kwa maelezo ya daktari Dkt. Lucas aliyoyatoa mahakamani kupingana na maelezo yake ya awali kwenye fomu namba tatu (PF.3) alipompima mtoto huyo mahakama ilishindwa kupata ukweli na hivyo kubaki na shaka kubwa iwapo kweli mshitakiwa alitenda kosa hilo na hivyo kumuachia huru.
 
Gasabile alisema hata hivyo mlalamikaji anayo haki ya kukata rufaa iwapo anaona hajatendewa haki na kwamba daima mahakama husimama katika kutenda haki na haiwezi kutoa adhabu kwa mshitakiwa iwapo ushahidi uliotolewa mahamani unatia shaka.
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top