Jamii ya Wahadzabe ni moja kati ya makabila yaliyobaki duniani yanayoendeleza shughuli za uwindaji, inadhaniwa kuwa jamii hii imeishi kaskazini mwa Tanzania, ikila matunda na mizizi, na aina mbalimbali za wanyama kwa miaka 40,000.
Mwandishi wa BBC, Dan Saladino alikwenda kuwashuhudia wakikusanya na kuwinda, na kuchunguza iwapo lishe yao ni suluhu kwa matatizo mengi yanayowasibu binadamu kwa sasa.
Angalizo: Baadhi ya picha ni za wanyama waliouawa ni huenda zikawa za kuogofya.
Wakati nikiwa nimelala kifudifudi, niliweka kichwa changu ndani ya shimo lenye giza nikahisi harufu ya mnyama
Lakini sikuamini kuwa mtu ataingia mle ndani na kumtoa mnyama huyo. Mtu huyo ni Zigwadzee, na mnyama alikuwa nungunungu, amini usiamini.
Baada ya kukabidhi uta, mshale na shoka lake kwa mwindaji mwenzake wa Hadzabe, Zigwadzee alishika fimbo fupi iliyochongoka na akaingia shimoni.

  • Zigwadzee heading down the porcupine hole
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top