Hapa Mukadam akiwa na mwenyekiti wa Kamati yake ya kampeni, Rashid Juma Mhango wakisubiri kutangazwa kwa matokeo katika kituo cha Tawi la CCM Nkomo.


 
Furaha ya ushindi, Mukadam akisindikizwa kuelekea nyumbani kupumzika baada ya kutangazwa mshindi.
ALIYEKUWA Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Gulam Hafeez Mukadam ameibuka na ushindi mkubwa katika kinyang’anyiro cha kura maoni zilizofanyika katika kata yake ya Mjini Shinyanga.


Wasimamizi wa uchaguzi huo wa kura za maoni ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika nchini kote Agosti mosi mwaka huu, walimtangaza Mukadam kuwa mshindi katika uchaguzi huo baada ya kupata jumla ya kura 247 katika matawi yote mawili ya kata ya mjini.

Mmoja wa wasimamizi wa kituo cha Tawi la Nkomo mjini Shinyanga, Ibrahimu Ramadhani alisema katika kituo hicho Mukadam alipata kura 182 akifuatiwa na mpinzani wake wa karibu Erasto Kwilasa aliyepata kura 53.

Mmoja wa wasimamizi wa uchaguzi katika kituo cha Tawi la CCM Nkomo, Ibrahimu Ramadhani akimtangaza rasmi Mukadam kuwa ndiye mshindi wa uchaguzi huo wa kura za maoni.


Wagombea wengine katika kituo hicho, Yusufu Mataba alipata kura nane, Salumu Abdalah Zamzam kura mbili na Willy Mzava ambaye ni mwenyekiti wa Umoja wa wazazi wa CCM mkoani Shinyanga aliambulia kura moja.

Katika kituo cha Tawi la CCM Mboya, aliyeongoza alikuwa ni Erasto Kwilasa kwa kupata kura 99 akifuatiwa na Mukadam aliyepata kura 65 huku wagombea Mzava akipata kura tano, Mataba kura mbili na Salum Abdalah Zamzam aliambulia kura mbili.
 
Mukadam akiondoka katika kituo cha kupigia kura cha Tawi la CCM Nkomo, kulia kwake ni Sheikh wa wilaya ya Shinyanga, Sheikh Suleiman Kategile.
Kutokana na matokeo hayo Mukadam ndiye mshindi wa jumla katika mchakato huo wa kura za maoni ambapo baadhi ya wanachama wa CCM wa kata ya Mjini waliwapongeza wasimamizi wa uchaguzi katika vituo vyote kwa jinsi walivyoendesha uchaguzi huo kwa uhuru na haki na hivyo mshindi kupatikana kwa haki.

Mara baada ya wasimamizi kumtangaza Mukadam kuwa ndiye mshindi wa jumla kwenye uchaguzi huo wa kura za maoni mamia ya wanachama wa CCM waliokuwa wakimuunga mkono mgombea huyo waliingia mitaani kwa shamra shamra kubwa wakishangilia kwa ushindi huo mnono.



Ni shamra shamra kwa kwenda mbele ni baada ya Mukadam kutangaza mshindi wa jumla katika uchaguzi wa kura za CCM udiwani kata ya Mjini Shinyanga

Kwa upande wa matokeo ya kura za maoni kwa wagombea kiti cha ubunge Jimbo la Shinyanga mjini, mbunge anayemaliza muda wake na Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Stephen aliongoza katika kata hiyo ya mjini.

Matokeo yaliyotangazwa katika kituo cha Tawi la CCM Nkomo, Masele alipata jumla ya kura 191 akifuatiwa na Erasto Kwilasa aliyepata kura 34, Hassan Fatiu (6), Charles Mlingwa (4), Abdalah Seni (4), Willy Mzava (1) na Mussa Ngangale (5) huku wagombea wawili Tara Nzeimana na Kazungu hawakuambulia hata kura moja.

Kituo cha Tawi la CCM Mboya, Masele alipata kura 85, Kwilasa 69, Mlingwa (5), Fatiu (4), Nzeimana (2), Mzava (8), Ngangale (4) Seni (5) na Kazungu hakuambulia kitu.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika baadhi ya kata mbalimbali ambazo hata hivyo hazijathibitishwa na mamlaka husika, mgombea Masele alikuwa akiongozi kwa kura nyingi katika vituo vyote vya kupigia kura.
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top