Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Jimbo la Mjini Mkongwe (CUF), Ismail Jussa (kulia) akiwa amemnyanyua mkono juu kada wa Chama cha CUF, Mansoor Yussuf Himid walipokuwa wakishiriki maandamano kuelekea kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja, mjini Unguja jana. Picha na Edwin Mjwahuzi 

CUF kimeendelea kupeperusha bendera ya zamani ya chama cha Afro Shiraz Party (ASP), ambacho kimefutwa kisheria baada ya kuungana na chama cha Tanu na kuzaliwa Chama cha Mapinduzi(CCM), Februari 5, 1977.


Bendera hiyo ya ASP ilipamba mkutano wa hadhara wa CUF uliofanyika jana kwenye uwanja wa Mnazi Mmoja ambako chama hicho kilikuwa kinazindua rasmi kamati za uchaguzi za chama hicho ambazo ni maalumu kwa ajili ya kushughulikia masuala yote yanayohusu uchaguzi mkuu ujao ikiwa ni pamoja na maandalizi.

Tofauti na ilivyozoeleka wafuasi wa chama hicho waliingia uwanjani hapo kwa makundi huku karibu kila mmoja akiwa amebeba bendera ya ASP, yenye rangi tatu za kijani, nyeusi na bluu bahari.

Kwa mujibu wa taarifa wafuasi wa CUF wameanza utaratibu wa kupeperusha bendera ya ASP kwa madai ya kuienzi Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK), na pia kutanguliza uzanzibari kwanza.

Hata hivyo siku za karibuni Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Zanzibar, Shaka Hamdu Shaka aliiomba Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kukichukulia hatua za kisheria chama cha CUF kwa madai ya kupeperusha bendera ya zamani ya chama ASP kinyume na sheria namba 5 ya mwaka 1992.

HALI NDIYO HIYO!!! WEWE MSOMAJI UNA MAONI GANI???
Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top