Aliyeuawa Simanjiro katika mgogoro wa Madaraka ya CCM, azikwa


Mchungaji wa Kanisa la KKKT akiendesha misa ya mazishi Nurueli Mbaga

Mgogoro wa kugombea madaraka ya uwenyekiti wa kijiji cha kambi ya chokaa wilayani Simanjiro umeingia katika uvunjifu wa amani baada ya mmoja wa wajumbe wa serikali ya kijiji anayemuunga mkono mgombea aliyependekezwa na CCM Mbiki Ratoi Bwana Yohana Rometi kuuawa kwa kupigwa na vitu vyenye ncha kali na wananchi wanaodaiwa kuunga mkono upande wa pili. 

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari mjumbe huyo wa serikali ya kijiji ambaye anatajwa kumuunga mkono mgombea mmoja kati ya wanaogombania nafasi hiyo anayedaiwa kuuawa na mashabiki wa upande wa pili katika vurugu zilizofanyika kijjijini hapo na kushuhudia watu waliojawa na huzuni huku wengine wakibubujikwa  machozi baada ya mwili wa marehemu Yohana Rometi kuwasili ukitokea hospitali ya KCMC mkoani Kilimanjaro. 

Akizungumza kifo hicho kaka wa marehemu Yohana Rometi Bwana John Rometi amesema tukio ilo limewatisha na anashindwa kuamini kuwa watanzania sasa wamefikia hatua ya kutoana uhai kwa ajili ya ushabiki wa kisiasa tena kwa chama kimoja huku akiiomba serikali itende haki na mmoja wa viongozi wa serikali ya kijiji hicho Kiberesa Kunei akiwataka familia ya marehemu kutolipiza kisasi kwani wameshaikabidhi serikali ili iweze kuchukua hatua.

Akihubiri katika ibada ya maziko mchungaji kiongozi wa kanisa la KKKT usharika wa Nomieuti wilaya ya Simanjiro Nurueli Mbaga amesema watanzania wa leo wamekuwa wabaya kuliko wanyama kwani dhulma, uonevu na ukatili vimeshika nafasi kuliko haki huku mwenyekiti aliyepitishwa na CCM anayedaiwa kuungwa mkono na marehemu ambaye ameapishwa Desemba 29 mwaka jana Mbuki Molel Ratoi akiwasii wananchi kuacha visasi kwa kuwa havina nafasi kwa sasa.

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Asante kwa kutembelea mtandao huu

Post a Comment

 
Top